Friday, April 27, 2012

Mji wa Manchester kuwaka moto

Hatumwi mtoto dukani. Ni msemo uliowahi kuusikia mara nyingi, lakini siku ya jumatatu utakua sahihi.

Ni siku ambapo wababe wawili wa Ligi kuu ya Premier ya England watapambana ikiwa ni kwenye uwanja wa Etihad wa Manchester City.
Baina ya timu hizi zimefunga bao 173 katika Ligi msimu huu tukishuhudia mengi yaliyofungwa na Wayne Rooney, Sergio Aguero, Javier Hernandez na Carlos Tevez.
uwanja wa City

Majina haya yanakupa ufahamu kua kila upande unaweza kufanikiwa kuchota pointi kutoka uwanja wa Etihad na kwa ushindi apo Etihad pia Ligi ya msimu huu.
Ukitazama orodha ya majina utaingiwa na tamaa ya ya pambano la kuvutia kutokana na washambuliaji wenye mikwaju mikali bila kusahau wanaowalisha mipira ya kupasua nyavu.

Man.City kwa kipindi kirefu imemtegemea David Silva na bado anaweza kushawishi matokeo ya mechi wakati wowote huku United ikimtegemea mno Antonio Valencia aliyekua na ushawishi mkubwa msimu huu kwa kuvunja ngome nyingi za vilabu mbalimbali.
.
David Silva
Vijana wa Roberto Mancini walipoteza muelekeo baada ya siku kuu ya Krisimasi kipindi ambapo kiwango cha mcheza kiungo David Silva kilianza kushuka ingawa hivi sasa klabu yake imerejesha uwezo wa kufunga mabao kutokana na hali yake kua bora kwa sasa.

Na huku kurejea kwa mshtuko kwa Paul Scholes mwezi januari kunaweza kuonekana kama changamoto iliyoiwezesha United kupanda kilele cha Ligi kuu, ingawa mchango wa Valencia kutoka upande wa kulia ni mkubwa mno. Valencia.

Kufuatia jeraha la kisiginio la mda mrefu mapema msimu huu Valenzia alizinduka kwa kupachika wavuni bao mbili kati ya 4-1 dhidi ya Wolves tarehe 10 Disemba.
Kwa uchache, hawa ni wawili kati ya orodha ndefu ya wachezaji wa Manchester mbili zinazotambiana kushinda pambano la jumatatu litakaloamua mshindi wa Ligi ya mwaka huu.
Antonio Valencia
Tuangalie uwezekano wa hali inayoweza kujitokeza ikiwa kwa mfano:
City itashinda - basi timu hizi mbili zitakua sawa kwa pointi kukisalia mechi mbili, wingi wa goli za City ukiiweka klabu hio juu ya kilele.
Droo -na hapa United itahitaji pointi nne kutoka mechi zilizobaki, hata ikiwa City itashinda mechi zote zilizobaki.

Hapa ushindi wa United katika mechi itakayofuata dhidi ya Swansea basi itatangazwa United kua mshindi endapo City itashindwa kuifunga Newcastle ugenini.
Endapo United itashinda pambano la jumatatu basi Ligi itahesabu kombe la 20 la United.

No comments:

Post a Comment