Mshatkiwa
Elizabeth Michael |(17), ' Lulu' akielekea kupanda ngazi na
kupandishwa Kizimbani Kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya kutajwa Upelelezi
haujakamilika hiyo ni kwa mujibu wa Wakili wa Serikali Elizabeth
Kaganda alisema mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo Rita Tarimo
hivyo kesi hiyo itatajwa tena Mei 7 mwaka huu. Mtuhumiwa amerudishwa rumande.
Akisindikizwa .
Mshtakiwa akipanda ngazi kuelekea
Kizimbani ambalo kesi yake ilitajwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi
Kisutu Jijini Dar es Salaam huku akiwa katika ulinzi kutoka kwa askari
Magereza.
Tofauti na ilivyokuwa alivyo pandishwa
kizimbani kwa mara ya kwanza 'Lulu' leo alikuwa katika ulizni wa hali
ya juu huku askari magereza wakiwa wamevalia mikanda yenye mabomu ya
machozi ikiwa ni katika kukabilia na rapsha ya aina yeyote ambayo
ingeweza kutokea .
Kitu kingine ni kwamba msanii huyo alifika akiwa
amevalia gauni refu na mtandio wake mwekundu walitu walijaa lakini siyo
kwa wingi ambao wengi walitarajia kutokana na umaarufu alio nao Lulu
hata kabla ya kufikwa na tuhuma hizo za kesi ya mauaji ya aliyekuwa
Msanii nyota wa Filamu nchini Steven Charles Kanumba.
No comments:
Post a Comment