Sunday, April 22, 2012

Kamati yapendekeza wabunge watungiwe kanuni za maadili

KAMATI ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge imependekeza wabunge watungiwe kanuni zinazohusu maadili ya wanasiasa hao ambazo zinaweka viwango kwa mienendo ya wabunge pale watakapokuwa wakitekeleza majukumu yao ya kibunge wawapo nje na katika eneo la Bunge.

Kamati hiyo inaeleza kuwa kwa sasa maadili ya wabunge ambayo yanasimamiwa kwa mujibu wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma, ambayo kwa madhumuni ya usimamizi bora wa maadili ya wabunge, sheria hiyo haikidhi haja ikiachiwa itumike peke yake.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Hassan Ngwilizi, kwenye taarifa hiyo anaeleza kuwa uzoefu unaonesha kuwa baadhi ya mabunge katika Jumuiya ya Madola tayari wana kanuni za maadili na mwenendo wa wabunge ambazo utafiti unaonesha kuwa kwa kiasi fulani kuwepo kwa kanuni hizo
kunaongeza imani ya wananchi kwa mabunge yao.

Malengo mengine ni kuwafanya wabunge kuonesha viwango vya juu vya maadili katika kutekeleza majukumu ya umma hususani wanapokuwa wakiisimamia Serikali.

No comments:

Post a Comment